No copying

Friday, 12 May 2017

MUNGU AMAWAPENDA WAMPENDAO TU


YESU ndiyo MUNGU aliye hai.

Karibu mtu wa MUNGU tujifunze neon la MUNGU.
Biblia takatifu inasema MUNGU anawapenda wale wampendao tu; kama humpendi MUNGU ina maana hawezi kukupenda pia.




  • Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. -MITHALI 8:17
 >>Huwezi kusiseme unampenda MUNGU wakati hulitii neno lake.
  • Mkinipenda, mtazishika amri zangu.- YOHANA 14:15
  • Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito. -1YOHANA 5:3
 >>Huwezi kusema unampenda MUNGU wakati hujamwamini YESU kama BWANA na MWOKOZI wa maisha yako.
  • Awapokeaye ninyi, anipokea mimi; naye anipokeaye mimi, ampokea yeye aliyenituma (MUNGU).---MATHAYO 10:40
 
 >>Huwezi kusema unampenda MUNGU wakati huwasikilizi watumishi wa MUNGU.
  • Awasikilizaye ninyi (watumishi wa Mungu)  anisikiliza mimi, naye awakataaye ninyi anikataa mimi; naye anikataaye mimi amkataa yeye aliyenituma.---LUKA 10:16

 >>Huwezi kuseme unampenda MUNGU wakati unamchukia YESU.
  • Yeye anichukiaye mimi humchukia na Baba yangu.--YOHANA 15:23
 
>>Huwezi kusema unampenda MUNGU wakati haumuheshimu YESU.
  •  Ili watu wote wamheshimu Mwana kama vile wanavyomheshimu Baba. Asiyemheshimu Mwana hamheshimu Baba aliyempeleka.--YOHANA 5:23
Asante kwa kusoma ujumbe huu mfupi.
Lakini nina neno moja kwako wewe ambaye hujaokoka au hujamwamini YESU.
Amua kumfuata na kumuamini ili upate uzima.

Ni mimi ndugu yako Faraja Euphrase
0757628749
farajaefraz@gmail.com
 

No comments:

 

Top

Back To Top
 
Blogger Templates